Maelfu ya wanawake katika Jamhuri ya Congo Brazzaville wameandamana
wakilalamikia mivutano ya kisiasa katika nchi yao. Maandamano hayo
makubwa yamefanyika katika mji mkuu Brazzaville. Waandamanaji hao
wametoa wito wa kuweko amani na uthabiti wa kisiasa katika nchi yao.
Wanawake wa Jamhuri ya Congo Brazzaville wamefanya maanadamo hayo
wakitaka kuweko utulivu wa kisiasa katika nchi yao baada ya kutokea
mvutano na mzozano baina ya serikali ya nchi hiyo na vyama vya upinzani.
Mvutano baina ya serikali ya Congo Brazzaville na vyama vya upinzani
umeshadidi baada ya pande mbili kutofautiana kuhusiana na marekebisho ya
katiba ya nchi hiyo. Uchaguzi wa Jamhuri ya Congo Brazzavile umepangwa
kufanyika mwaka ujao. Kwa mujibu wa Katiba ya nchi hiyo, ukomo wa
uongozi wa Rais ni duru mbili tu na Rais wa nchi hapaswi kuwa na zaidi
ya miaka sabini. Agosti mwaka ujao Rais Denis Sassou Nguesso
anakamilisha duru mbili za uongozi hivyo kwa mujibu wa katiba ya nchi
hapaswi kugombea katika uchaguzi ujao
0 comments:
Post a Comment