Bunge la Libya, lililochaguliwa na wananchi limekubali kurudi katika majadiliano ya amani yanayofadhiliwa na Umoja wa Mataifa.
Kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters, hii ni wiki moja baada ya
kujitoa na mjumbe wa Bunge linalohasimiana kusema mazungumzo
yanatarajiwa kuanza siku ya Alhamisi.
Mataifa ya magharibi yanaona mazungumzo ya Umoja wa Mataifa kama
nafasi pekee ya kumaliza mzozo wa Libya wa kugombania madaraka kati ya
serekali mbili pinzani na majeshi yao.
Hali ya kutoelewana inaweza kuhatarisha kuipeleka nchi hiyo katika
vita zaidi ya wenyewe kwa wenyewe inayokaribia miaka minne sasa tangu
kuondolewa kwa utawala wa Muammar Gaddafi.
Wakati huo huo, Khalifa Haftar, kiongozi muhimu katika mapinduzi ya
Libya amechaguliwa kuwa mkuu wa jeshi la serikali inayotambulika
kimataifa.
Uteuzi wa Haftar unaonekana unaweza kuleta taharuki katika mazungumzo
hayo ya Umoja wa Mataifa ya kujaribu kumaliza mzozo wa nchi hiyo
0 comments:
Post a Comment