Tuesday, 3 March 2015

Majeshi ya Chad, yamevurumusha wanamgambo wa Boko Haram, kutoka mji wa Dikwa, kaskazini mashariki mwa Nigeria, na kupoteza mwanajeshi mmoja katika mapambano kwa mujibu wa msemaji wa jeshi.
Shirika la habari la Reteuters linaripoti kwamba  Chad imepeleka maelfu ya wanajeshi wake katika maeneo muhimu  kuzunguka ziwa Chad.
Hizo ni hatua za kupambana na wanamgambo wenye msimamo mkali ndani ya Nigeria, na wakati mwengine kuvuka mipaka.
Hatua hiyo imechochewa toka wanamgambo wa Boko Haram, waliposhambulia kijiji cha Chad, cha Ngouboua, mwezi uliopita na kuua watu kadhaa katika shambulio la kwanza kufahamika lililosababisha vifo nchini humo

WATOTO WAANDIKISHWA KUJIUNGA NA JESHI

Umoja wa mataifa unaeleza kwamba hivi sasa unahofu kuwa mamia ya wavulana waliotekwa mwezi uliopita Sudan Kusini, wameandikishwa kwa nguvu kuwa wanajeshi.
Msemaji wa Umoja wa Mataifa, Stephane Dujarric, amesema shirika la Umoja wa Mataifa la kushughulikia watoto UNICEF, linaamini idadi ya watoto waliotekwa katika jimbo la Upper Nile ni zaidi ya 89 tofati na ilivyoripotiwa.
UNICEF inaamini watoto hao waliotekwa wanatoka kundi la wanamgambo wenye uhusiano na jeshi la Sudan Kusini.
Inauhakika kundi lenye silaha linaongozwa na Johson Oloni, Jenerali ambaye alipigana dhidi ya serikali, lakini wanamgambo wake sasa wanauhusiano na jeshi la kitaifa.
Mashuhuda wanasema watu wenye silaha walizunguka kijiji cha Wu Shilluk, na kwenda nyumba kwa nyumba kutafua wavulana waliodhaniwa kuwa na miaka 12 na zaidi.
UNICEF inasema pia watu wazima walilazimishwa kujiunga na jeshi hilo.

0 comments:

Post a Comment

Translate

facebook

TANGAZA HAPA

KWA HABARI MAKINI

Napokea maoni muhimu kwa pale unapoona apakustahili kuwepo kwenye blogg yetu makini yenye lengo la kukuunganisha pamoja na kuelimishana kwa yale mazuri yote piga simu kwa chochote muhimu namba zipo apo juu

NEWS