Majeshi ya Chad, yamevurumusha wanamgambo wa Boko Haram, kutoka mji
wa Dikwa, kaskazini mashariki mwa Nigeria, na kupoteza mwanajeshi mmoja
katika mapambano kwa mujibu wa msemaji wa jeshi.
Shirika la habari la Reteuters linaripoti kwamba Chad imepeleka maelfu ya wanajeshi wake katika maeneo muhimu kuzunguka ziwa Chad.
Hizo ni hatua za kupambana na wanamgambo wenye msimamo mkali ndani ya Nigeria, na wakati mwengine kuvuka mipaka.
Hatua hiyo imechochewa toka wanamgambo wa Boko Haram, waliposhambulia kijiji cha Chad, cha Ngouboua, mwezi uliopita na kuua watu kadhaa katika shambulio la kwanza kufahamika lililosababisha vifo nchini humo
WATOTO WAANDIKISHWA KUJIUNGA NA JESHI
Shirika la habari la Reteuters linaripoti kwamba Chad imepeleka maelfu ya wanajeshi wake katika maeneo muhimu kuzunguka ziwa Chad.
Hizo ni hatua za kupambana na wanamgambo wenye msimamo mkali ndani ya Nigeria, na wakati mwengine kuvuka mipaka.
Hatua hiyo imechochewa toka wanamgambo wa Boko Haram, waliposhambulia kijiji cha Chad, cha Ngouboua, mwezi uliopita na kuua watu kadhaa katika shambulio la kwanza kufahamika lililosababisha vifo nchini humo
WATOTO WAANDIKISHWA KUJIUNGA NA JESHI
Umoja wa mataifa unaeleza kwamba hivi sasa unahofu kuwa mamia ya
wavulana waliotekwa mwezi uliopita Sudan Kusini, wameandikishwa kwa
nguvu kuwa wanajeshi.
Msemaji wa Umoja wa Mataifa, Stephane Dujarric, amesema shirika la Umoja wa Mataifa la kushughulikia watoto UNICEF, linaamini idadi ya watoto waliotekwa katika jimbo la Upper Nile ni zaidi ya 89 tofati na ilivyoripotiwa.
UNICEF inaamini watoto hao waliotekwa wanatoka kundi la wanamgambo wenye uhusiano na jeshi la Sudan Kusini.
Inauhakika kundi lenye silaha linaongozwa na Johson Oloni, Jenerali ambaye alipigana dhidi ya serikali, lakini wanamgambo wake sasa wanauhusiano na jeshi la kitaifa.
Mashuhuda wanasema watu wenye silaha walizunguka kijiji cha Wu Shilluk, na kwenda nyumba kwa nyumba kutafua wavulana waliodhaniwa kuwa na miaka 12 na zaidi.
UNICEF inasema pia watu wazima walilazimishwa kujiunga na jeshi hilo.
Msemaji wa Umoja wa Mataifa, Stephane Dujarric, amesema shirika la Umoja wa Mataifa la kushughulikia watoto UNICEF, linaamini idadi ya watoto waliotekwa katika jimbo la Upper Nile ni zaidi ya 89 tofati na ilivyoripotiwa.
UNICEF inaamini watoto hao waliotekwa wanatoka kundi la wanamgambo wenye uhusiano na jeshi la Sudan Kusini.
Inauhakika kundi lenye silaha linaongozwa na Johson Oloni, Jenerali ambaye alipigana dhidi ya serikali, lakini wanamgambo wake sasa wanauhusiano na jeshi la kitaifa.
Mashuhuda wanasema watu wenye silaha walizunguka kijiji cha Wu Shilluk, na kwenda nyumba kwa nyumba kutafua wavulana waliodhaniwa kuwa na miaka 12 na zaidi.
UNICEF inasema pia watu wazima walilazimishwa kujiunga na jeshi hilo.
0 comments:
Post a Comment