Thursday, 19 March 2015

Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania ameziagiza mamlaka za ulinzi na usalama nchini humo
  Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania ameziagiza mamlaka za ulinzi na usalama nchini humo kuhakikisha shughuli ya kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura na upigaji kura ya Katiba Inayopendekezwa unafanyika kwa amani na wasioitakia mema nchi wasibadilishe matukio hayo kuwa fujo na kuingiza nchi kwenye vurugu. Rais Kikwete amesema, kazi ya kuboresha daftari la wapiga kura, imeanzia Njombe na itaendelea mikoa mingine na kuwataka viongozi hao kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi na kukumbusha maana ya kuwa na kitambulisho cha kura ambacho kitamwezesha kupiga kura ya maoni na katika uchaguzi mkuu mwaka huu. Rais wa Tanzania amezungumzia tena suala la mauaji ya albino, usafirishaji wa madawa ya kulevya na kubainisha kwamba, ni jambo la aibu, kijinga na fedheha kubwa kwa mtu mzima na akili zake kuamini kwamba, akipata kidole cha albino mambo yake yatamnyookea na kupata mafanikio ya maisha. Rais Kikwete amezitaka kamati za ulinzi na usalama za Tanzania zikae na kuona namna zitavyokabiliana na suala hilo. Wakati huo huo, utata umegubika uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi Tanzania baada ya Serikali kutaka kuwasilisha ‘kinyemela’ muswada wa uanzishwaji wa mahakama hiyo, kwenye Mkutano huu wa 19 wa Bunge unaoendelea  mjini Dodoma bila kuupitisha kwenye Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala kama utaratibu unavyotaka.

0 comments:

Post a Comment

Translate

facebook

TANGAZA HAPA

KWA HABARI MAKINI

Napokea maoni muhimu kwa pale unapoona apakustahili kuwepo kwenye blogg yetu makini yenye lengo la kukuunganisha pamoja na kuelimishana kwa yale mazuri yote piga simu kwa chochote muhimu namba zipo apo juu

NEWS