Friday, 12 December 2014

 ICC yaitaka Ivory Coast imkabidhi Simone Gbagbo
Majaji wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC wameitaka serikali ya Ivory Coast imkabidhi kwenye korti hiyo Simone Gbagbo, mke wa rais wa zamani wa nchi hiyo, ili akashtakiwe kutokana na tuhuma zinazomkabili.
Mwanamama huyo aliyekuwa anashikiliwa nyumbani juzi alihamishiwa mjini Abdjan kwa ajili ya kusikilizwa kesi yake nchini humo. Ivory Coast imekataa kumkabidhi na kusema kuwa itamhukumu nyumbani.
Tayari rais wa zamani wa nchi hiyo Laurent Gbagbo na Charles Ble Goude mtu wa karibu wa Gbagbo wameshafikishwa mbele ya Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC mjini The Hague Uholanzi. Watatu hao wanakabiliwa na tuhuma za kuchochea mapigano ya ndani nchini Ivory Coast yaliyopelekea watu 3,000 kuuawa,  baada ya uchaguzi wa rais wa mwaka 2010.

0 comments:

Post a Comment

Translate

facebook

TANGAZA HAPA

KWA HABARI MAKINI

Napokea maoni muhimu kwa pale unapoona apakustahili kuwepo kwenye blogg yetu makini yenye lengo la kukuunganisha pamoja na kuelimishana kwa yale mazuri yote piga simu kwa chochote muhimu namba zipo apo juu

NEWS