Polisi nchini Afrika Kusini imesema inachunguza tuhuma za ufisadi dhidi ya Rais wa nchi hiyo, Jacob Zuma.
Taarifa ya polisi kwa Bunge imekiri kwamba uchunguzi huo
umeanzishwa na unajikita zaidi katika madai kwamba, Rais Zuma alitumia
takriban dola milioni 24 kwa ajili ya kukarabati nyumba yake ya
kibinafsi katika eneo la Nkandia. Fedha hizo zinazodaiwa kuwa mali ya
umma zinasemekana zimetumika kujenga vitu vya anasa na starehe nyumbani
kwa Rais Zuma kama vile ukumbi wa densi na bwawa la kuogelea.
Tayari upinzani umemtaka kiongozi huyo ajiuzulu kufuatia
kashfa hiyo. Hata hivyo Rais Zuma amesema hakufahamishwa kuhusu
marekebisho hayo kwenye nyumba yake. Waliosimamia shughuli hiyo wamesema
vitu vilivyoongezwa kwenye nyumba ya Zuma vinahusiana na usalama kama
inavyotakiwa kisheria na hakuna fedha za umma zilizofujwa.
0 comments:
Post a Comment