Thursday, 2 October 2014

Waziri wa Mambo ya Nje wa China Wang Yi ameitahadharisha Marekani na nchi nyinginezo na kuzitaka zisiingilie maandamano yanayoendelea katika mji wa Hong Kong, na kusema kuwa maandamano hayo si halali. Wangi Yi amesema hayo alipokutana na mwenzake wa Marekani John Kerry kabla ya kukutana huko white House na Rais Barack Obama.
Maandamano yameendelea kushuhudiwa kwa siku 4 katika mji wa kibiashara wa Hong Kong, huku baadhi ya mashule, vituo vya biashara na mabenki yakifungwa. Maandamano hayo yalianza baada ya serikali ya China kukataa uchaguzi wa wazi wa kiongozi wa mji huo katika uchaguzi ujao wa mwaka 2017, na kulazimisha wapiga kura wachague kutoka katika orodha ya wagombea wawili au watatu watakaopitishwa na kamati ya uteuzi. Waandamanaji hao wameapa kuendelea na maandamano hadi pale kiongozi wa Hong Kong CY Leung atakapojiuzulu.

0 comments:

Post a Comment

Translate

facebook

TANGAZA HAPA

KWA HABARI MAKINI

Napokea maoni muhimu kwa pale unapoona apakustahili kuwepo kwenye blogg yetu makini yenye lengo la kukuunganisha pamoja na kuelimishana kwa yale mazuri yote piga simu kwa chochote muhimu namba zipo apo juu

NEWS