Wednesday, 24 September 2014

Watu 70 wakiwemo wanasiasa mashuhuri wamekabidhi fomu zao kwa Kamati Kuu ya Uchaguzi ya Tunisia kwa ajili ya kugombea kiti cha rais wa nchi hiyo. Huo utakuwa uchaguzi wa pili wa rais nchini Tunisia baada ya kung'olewa madarakani dikteta wa zamani wa nchi hiyo Zainul Abidin bin Ali.
Katika majina ya waliojiandikisha kwa ajili ya kiti cha raia wa Tunisia wamo baadhi ya mawaziri na maafisa wa utawala wa zamani wa nchi hiyo. Hii ni mara ya kwanza katika historia ya Tunisia kushuhudiwa idadi kubwa kama hiyo ya watu waliojiandikisha kugombea kiti cha rais.
Sheria za uchaguzi za Tunisia zinamlazimisha mgombea yeyote wa kiti cha rais kuungwa mkono na watu wasiopungua elfu kumi au wabunge 10. Duru ya kwanza ya uchaguzi wa Rais wa Tunisia itafanyika tarehe 23 Novemba na iwapo hatapatikana mshindi duru ya pili ya uchaguzi huo imepangwa kufanyika tarehe 28 Disemba. Uchaguzi wa Bunge wa Tunisia pia utafanyika tarehe 26 Oktoba.

Related Posts:


0 comments:

Post a Comment

Translate

facebook

TANGAZA HAPA

KWA HABARI MAKINI

Napokea maoni muhimu kwa pale unapoona apakustahili kuwepo kwenye blogg yetu makini yenye lengo la kukuunganisha pamoja na kuelimishana kwa yale mazuri yote piga simu kwa chochote muhimu namba zipo apo juu