Kundi la waasi wa Jamhuri ya Afrika ya Kati limewateka nyara raia tisa
wa Cameroon kwa shabaha ya kuishinikiza serikali ya nchi hiyo imuachilie
huru kiongozi wa waasi hao aliyeko jela nchini Cameroon. Gazeti la
Mutations linalochapishwa Cameroon limeandika kuwa, waasi wa Jamhuri ya
Afrika ya Kati wametishia kwamba, iwapo serikali ya Cameroon
haitamuachilia huru Abdallah Miskin katika kipindi cha masaa 72,
wataanzisha mashambulizi makali ndani ya ardhi ya Cameroon. Abdallah
Miskin ni mmoja wa viongozi wa matawi ya harakati ya Seleka huko Jamhuri
ya Afrika ya Kati. Inafaa kuashiria hapa kuwa, Abdallah Miskin alitiwa
mbaroni na kufungwa jela mwaka jana nchini Cameroon, baada ya kushadidi
mapigano kati ya wanamgambo wa Seleka na kundi la wanamgambo wa Kikristo
la Anti Balaka. Mgogoro wa Jamhuri ya Afrika ya Kati umepatiwa
ufumbuzi, baada ya makundi hasimu nchini humo kufikia makubaliano ya
amani yaliyosainiwa miezi michache iliyopita huko Brazzaville, Jamhuri
ya Kongo.
Tuesday, 23 September 2014
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment