Wednesday, 24 September 2014

Bunge la Libya limeliidhinisha baraza jipya la mawaziri lililoteuliwa na Waziri Mkuu wa nchi hiyo Abdullah al Thani baada ya kulikataa lile la awali aliloliteuwa wiki iliyopita. Baraza jipya la mawaziri la Libya lililoidhinishwa jana na bunge linawajumuisha mawaziri 13 na Manaibu Waziri Mkuu watatu. Wabunge wa Libya walilikataa baraza la mawaziri la awali lililokuwa na mawaziri 18 na kumtaka Waziri Mkuu Abdullah al Thani ateuwe timu ya mawaziri wachache.
Abdullah al Thani ambaye alikuwa akikaimu nafasi ya Waziri Mkuu wa Libya tangu mwezi Machi mwaka huu, alijiuzulu baada ya uchaguzi wa mwezi Juni; na mwanzoni mwa mwezi huu bunge jipya la Libya lilimteuwa tena kushika nafasi hiyo. Weledi wa mambo wanasema kuwa al Thani hata hivyo ameshindwa kurejesha utulivu huko Libya, nchi ambayo imekuwa ikikabiliwa na machafuko kwa karibu miaka mitatu sasa baada ya kuanguka utawala wa kiongozi wa zamani wa nchi hiyo Kanali Muammar Gaddafi.

0 comments:

Post a Comment

Translate

facebook

TANGAZA HAPA

KWA HABARI MAKINI

Napokea maoni muhimu kwa pale unapoona apakustahili kuwepo kwenye blogg yetu makini yenye lengo la kukuunganisha pamoja na kuelimishana kwa yale mazuri yote piga simu kwa chochote muhimu namba zipo apo juu

NEWS