Naibu Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Iran amesema kuwa, Tehran ina
shaka na nia ya Marekani ya
Naibu Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Iran amesema kuwa, Tehran ina
shaka na nia ya Marekani ya kutaka kupambana na ugaidi. Akizungumza na
ujumbe wa maseneta kutoka nchini Kenya ulioko nchini, Hussein Amir
Abdulahiyan amesema kuwa, mara baada ya kuanza mgogoro wa Syria, Iran
ilizitahadharisha nchi za Magharibi juu ya matokeo mabaya na hatari ya
kuyaunga mkono makundi ya kigaidi. Abdulahiyan ameongeza kuwa, baada ya
kupita muongo mmoja makundi yanayofungamana na al Qaeda yamekuwa na
uzoefu mkubwa katika kutekeleza operesheni zao za kigaidi katika nchi za
Afghanistan na Iraq. Naibu Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Iran
amesema kuwa, uhusiano wa Tehran na Nairobi uko katika kiwango kizuri,
na kusisitiza kwamba nafasi ya mabunge na hasa Kamisheni ya Usalama wa
Taifa na Sera za Kigeni ina nafasi muhimu mno. Kwenye mazungumzo hayo,
Muhammad Yussuf Haji, Mkuu wa Kamisheni ya Usalama wa Taifa na Sera za
Kigeni katika Bunge la Seneti la Kenya ameelezea azma ya serikali ya
nchi yake ya kuimarisha mashirikiano na Iran na kusisitiza kwamba
Nairobi ina taarifa za kutosha kuhusu hatua kubwa za maendeleo
zilizopigwa na Iran katika nyanja za elimu na teknolojia. Haji ameongeza
kuwa, Kenya inataka mashirikiano ya pande mbili katika nyanja
mbalimbali yaimarishwe zaidi.kutaka kupambana na ugaidi. Akizungumza na
ujumbe wa maseneta kutoka nchini Kenya ulioko nchini, Hussein Amir
Abdulahiyan amesema kuwa, mara baada ya kuanza mgogoro wa Syria, Iran
ilizitahadharisha nchi za Magharibi juu ya matokeo mabaya na hatari ya
kuyaunga mkono makundi ya kigaidi. Abdulahiyan ameongeza kuwa, baada ya
kupita muongo mmoja makundi yanayofungamana na al Qaeda yamekuwa na
uzoefu mkubwa katika kutekeleza operesheni zao za kigaidi katika nchi za
Afghanistan na Iraq. Naibu Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Iran
amesema kuwa, uhusiano wa Tehran na Nairobi uko katika kiwango kizuri,
na kusisitiza kwamba nafasi ya mabunge na hasa Kamisheni ya Usalama wa
Taifa na Sera za Kigeni ina nafasi muhimu mno. Kwenye mazungumzo hayo,
Muhammad Yussuf Haji, Mkuu wa Kamisheni ya Usalama wa Taifa na Sera za
Kigeni katika Bunge la Seneti la Kenya ameelezea azma ya serikali ya
nchi yake ya kuimarisha mashirikiano na Iran na kusisitiza kwamba
Nairobi ina taarifa za kutosha kuhusu hatua kubwa za maendeleo
zilizopigwa na Iran katika nyanja za elimu na teknolojia. Haji ameongeza
kuwa, Kenya inataka mashirikiano ya pande mbili katika nyanja
mbalimbali yaimarishwe zaidi.
Tuesday, 23 September 2014
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment