Tuesday, 23 September 2014

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo amesema kuwa, ugonjwa wa ebola ambao unaendelea kusambaa kwa kasi katika eneo la magharibi mwa Afrika, umeweza kudhibitiwa kwa kiasi kikubwa nchini Kongo. Augustin Matata Ponyo amesema kuwa, katika siku za hivi karibuni hakujashuhudiwa kesi yoyote inayohusiana na maradhi ya ebola nchini humo. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo amesema kuwa, idadi ya watu waliopatwa na maradhi hayo kuanzia mwezi uliopita hadi sasa ni 68, na wengine 41 wameshafariki dunia kutokana na ugonjwa huo. Inafaa kuashiria hapa kuwa, kwa mujibu wa takwimu za Shirika la Afya Duniani WHO, zaidi ya watu 2,700 wameshafariki dunia hususan katika nchi za Liberia, Guinea na Sierra Leone kutokana na maradhi ya ebola.

0 comments:

Post a Comment

Translate

facebook

TANGAZA HAPA

KWA HABARI MAKINI

Napokea maoni muhimu kwa pale unapoona apakustahili kuwepo kwenye blogg yetu makini yenye lengo la kukuunganisha pamoja na kuelimishana kwa yale mazuri yote piga simu kwa chochote muhimu namba zipo apo juu

NEWS