Mwakilishi maalumu wa Umoja wa
Mataifa katika masuala ya Yemen amesema kuwa, vyombo vya ulinzi na
usalama vya nchi hiyo vimesambaratika kikamilifu. Akizungumza mjini
Sana'a, Jamal bin Omar amesisitiza kwamba vyombo vya ulinzi na usalama
vya Yemen vimesambaratika na hata katika baadhi ya maeneo ya nchi hiyo
hakuna usalama kabisa na maeneo mengine yanadhibitiwa kikamilifu na
makundi ya wanamgambo wanaobeba silaha.
Wakati huohuo, Wizara ya Afya ya Yemen
imetangaza kuwa, kwa akali watu 200 wameuawa na wengine 461 kujeruhiwa
baada ya kujiri mapigano hivi karibuni mjini Sana'a kati ya wanaharakati
wa al Houthi na wafuasi wa chama cha al Islaah, kinachoungwa mkono na
jeshi la nchi hiyo. Taarifa zaidi zinasema kuwa, usalama umeshaanza
kurejea tena kwa kiwango fulani nchini Yemen, baada ya kutiwa saini
makubaliano ya kisiasa na ya amani kati ya Rais wa Yemen na harakati ya
al Houthi.
0 comments:
Post a Comment