Duru za Habari zimefichua kuwa, Rais wa Mamlaka ya Ndani ya
Palestina, Mahmoud Abbas, katika miezi ya hivi karibuni amekuwa
akishinikizwa na Marekani akubali kuanza tena mazungumzo eti ya amani na
utawala haramu wa Israel. Habari zinasema kuwa, Waziri wa Mambo ya Nje
wa Marekani, John Kerry, amemtaka Mahmoud Abbas kuunda mara moja timu
mpya kwa ajili ya duru nyingine ya mazungumzo na Israel. Imeripotiwa
kuwa, Kerry anashinikiza mazungumzo mapya kuanza mwezi ujao wa Oktoba
kati ya ujumbe wa Palestina na ule wa Wazayuni. Pia kuna mpango wa
kuwakutanisha tena Benjamin Netanyahu, Waziri Mkuu wa utawala bandia wa
Israel, Mahmoud Abbas na Rais Barack Obama wa Marekani huko Washington
baadaye mwaka huu.
Tangu kuanza mazungumko kati ya Israel na Mamlaka ya Ndani ya Palestina mwaka 1991, Wazayuni wamekuwa wakivuta wakati na kuendelea kupora ardhi za Wapalestina na kwa njia hiyo, mazungumzo hayo yameshindwa kufikia natija yoyote. Makundi ya wanamapambano wa Palestina yamekuwa yakisisitiza mara kwa mara kuwa, mazungumzo na Wazayuni hayana manufaa yoyote kwa Wapalestina na njia pekee ya kupata haki ni kupitia mapambano ya silaha dhidi ya utawala huo ghasibu.
Tangu kuanza mazungumko kati ya Israel na Mamlaka ya Ndani ya Palestina mwaka 1991, Wazayuni wamekuwa wakivuta wakati na kuendelea kupora ardhi za Wapalestina na kwa njia hiyo, mazungumzo hayo yameshindwa kufikia natija yoyote. Makundi ya wanamapambano wa Palestina yamekuwa yakisisitiza mara kwa mara kuwa, mazungumzo na Wazayuni hayana manufaa yoyote kwa Wapalestina na njia pekee ya kupata haki ni kupitia mapambano ya silaha dhidi ya utawala huo ghasibu.
0 comments:
Post a Comment