Nchi kadhaa za Kiarabu zimependekeza rasimu ya azimio dhidi ya
silaha za nyuklia za utawala wa Kizayuni wa Israel katika mkutano wa
Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA). Utangulizi huo wa
azimio linaloungwa mkono na nchi 18 za Kiarabu, umeelezea wasiwasi
mkubwa juu ya uwezo wa nyuklia wa utawala wa Kizayuni na kuitaka Israel
ijiunge na Mkataba wa Kuzuia Kuzalisha na Kusambaza Silaha za Nyuklia
(NPT).
Israel ambayo ndio utawala pekee wenye kuhodhi silaha za nyuklia katika Mashariki ya Kati, inaripotiwa kuwa na vichwa kati ya 200 hadi 400 vya mabomu ya nyuklia. Zaidi ya hayo, Israel haijawahi kuruhusu kukaguliwa viwanda vyake vya nyuklia na inaendelea kupuuza wito wa kimataifa wa kujiunga na mkataba wa NPT.
Israel ambayo ndio utawala pekee wenye kuhodhi silaha za nyuklia katika Mashariki ya Kati, inaripotiwa kuwa na vichwa kati ya 200 hadi 400 vya mabomu ya nyuklia. Zaidi ya hayo, Israel haijawahi kuruhusu kukaguliwa viwanda vyake vya nyuklia na inaendelea kupuuza wito wa kimataifa wa kujiunga na mkataba wa NPT.
0 comments:
Post a Comment