Wizara ya Mambo ya Nje ya Misri
imetangaza kuwa Wapalestina na Israel wamekubaliana kuendeleza
mazungumzo kuhusiana na makubaliano ya usitishaji vita. Mahmoud al Zahar
mmoja wa viongozi wa harakati ya Hamas ya Palestina pia ameeleza kuwa
ujumbe wa Palestina umeamua kuendeleza vikao vya Cairo baada ya
kushauriana na wanachama wa harakati hiyo ndani na nje ya Ghaza.
Kabla ya hapo, baadhi ya duru za habari
za Palestina ziliripoti kuwa, ujumbe wa Palestina unachunguza kujiengua
kwenye mazungumzo ya Cairo ikiwa ni jibu na radiamali kwa kuuliwa
wanachama wawili wa muqawama huko al Khalil. Wazayuni ambao wanadai
kuwa Amar Abu Aisha na Marwan al Qawasmih wanachama wa brigedi za
Izzuddin al Qassam tawi la kijeshi la Hamas walihusika kuwateka nyara na
kuwauwa walowezi watatu wa Kizayuni huko al Khalil, jana asubuhi
waliwaua shahidi wanaharakati hao.
0 comments:
Post a Comment