Wednesday, 24 September 2014

Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza juu ya udharura wa kushirikiana nchi za eneo la Mashariki ya Kati ili kuyapatia ufumbuzi matatizo ya mazingira ya eneo hili.  Rais Hassan Rouhani amesisitiza juu ya udharura wa kushirikiana nchi za eneo ili kutatua matatizo ya mazingira na kusisitiza kuwa mazingira na usalama wa watu kamwe haviwezi kukabiliwa na hatari kutokana na vikwazo vilivyo kinyume cha sheria, iwapo kutakuweko na mtazamo wa pamoja wa kibinadamu na kulifanya suala la usalama kuwa mhimili mkuu. Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameyasema hayo katika hotuba aliyoitoa jana mjini New York kwenye kikao cha wakuu wa nchi kuhusu mabadiliko ya tabia nchi.
Rais Hassan Rouhani  amekitaja kikao hicho cha wakuu wa nchi kuhusu mabadiliko ya tabia nchi kuwa ni fursa nzuri ya kuzungumzia mabadiliko ya tabia nchi  kama moja ya changamoto muhimu za karne ya 21 na kueleza kuwa,  ongezeko la joto duniani na athari zake za kupungua mvua katika eneo la Mashariki ya Kati, ukame wa mfululizo na kupungua maji, yamezidisha umaskini na kupelekea uwezekano wa kuibuka machafuko na mivutano ya mpakani; hata hivyo akasema kuwa kwa bahati mbaya kuendelea mizozo ya kisiasa na vita katika nchi jirani pia kumekuwa kikwazo cha kufikiwa makubaliano ya kivitendo na ya kudumu kwa ajili ya kutatua matatizo ya mazingira katika eneo hili. Dakta Hassan Rouhani amesema pia kwamba kuibuliwa vizingiti vya aina yoyote katika njia ya ushirikiano wa nchi za ulimwengu katika  kutatua matatizo ya mazingira kutakuwa kwa madhara ya jamii ya kimataifa.
Wakati huo huo Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran jana pia alikutana na kufanya mazungumzo na Rais Recep Tayyep Erdogan wa Uturuki pambizoni mwa mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa huko New York. Katika mazungumzo hayo Marais wa Iran na Uturuki walishauriana juu ya njia ya kuimarisha uhusiano kati ya nchi mbili hizo. Mbali na Rais wa Uturuki, Rais Hassan Rouhani alikuwa na mazungumzo pia na Rais wa Ufaransa, Venezuela na viongozi wengine kadhaa.  

0 comments:

Post a Comment

Translate

facebook

TANGAZA HAPA

KWA HABARI MAKINI

Napokea maoni muhimu kwa pale unapoona apakustahili kuwepo kwenye blogg yetu makini yenye lengo la kukuunganisha pamoja na kuelimishana kwa yale mazuri yote piga simu kwa chochote muhimu namba zipo apo juu

NEWS