Wednesday, 24 September 2014

Viongozi wa dunia wameahidi dola bilioni 2.3 katika mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi, kwa lengo la kusaidia maendeleo ya nchi katika kukabiliana na madhara yanayotokana na ongezeko la joto la dunia.  Mwishoni mwa kikao hicho Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon ametoa wito wa kufanywa jitihada za kufikiwa makubaliano ya dunia ya tabianchi ifikapo mwaka kesho, na kuwataka viongozi wa dunia watekeleze majukumu yao katika kulinda sayari ya dunia kwa kupunguza joto la dunia kwa  nyuzi joto 2.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa pia ametaka viongozi wa dunia wachukue hatua zaidi za kupunguza gesi za nyumba ya kioo, kuzuia kukatwa misitu na kusaidia nchi masikini kukabiliana na madhara ya mabadiliko ya hali ya hewa kama vile ukame, mafuriko, vimbunga na kupanda kiwango cha maji ya bahari.
Kwa muda mrefu sasa nchi zinazoendelea zimekuwa zikitaka kusaiiniwe makubaliano kuhusu tabianchi bila kujali ahadi za Marekani, zikisema kuwa nchi hiyo tajiri na iliyoendelea ndiyo inayochangia pakubwa katika kuharibu hali ya hewa duniani.

0 comments:

Post a Comment

Translate

facebook

TANGAZA HAPA

KWA HABARI MAKINI

Napokea maoni muhimu kwa pale unapoona apakustahili kuwepo kwenye blogg yetu makini yenye lengo la kukuunganisha pamoja na kuelimishana kwa yale mazuri yote piga simu kwa chochote muhimu namba zipo apo juu

NEWS