Tuesday, 30 September 2014

“Qatar iwekewe vikwazo kwa kuunga mkono ugaidi”

Mkuu wa Kamati ya Ujasusi na Usalama katika Bunge la Uingereza ametaka serikali ya Qatar iwekewe vikwazo. Sir Malcolm Rifkind amesisitiza kuwa, Uingereza na nchi nyingine za Ulaya zinapasa kuiwekea vikwazo Qatar na nchi nyingine za Kiarabu kutokana na uungaji mkono wao wa kifedha kwa makundi ya kigaidi. Rifkind ameongeza kuwa, Jonathan Shaw mmoja wa majenerali wa zamani wa Uingereza alisema hivi karibuni kwamba baadhi ya nchi za Kiarabu za eneo la Ghuba ya Uajemi zinaunda makundi ya kigaidi ndani ya nchi zao. Mkuu wa Kamati ya Ujasusi na Usalama ya Bunge la Uingereza amesema kuwa, kuna ulazima wa kuelezwa kinagaubaga viongozi wa Qatar kwamba, uhusiano wa kiuchumi wa London na Doha utakatika iwapo serikali ya Qatar itaendelea kuwaunga mkono magaidi. Sir Malcolm Rifkind amebainisha kuwa, nchini Qatar kuna vile alivyoviita 'vituo vya hisani' ambavyo hujishughulisha na ukusanyaji fedha kwa ajili ya makundi ya kigaidi na hata kuna baadhi ya makundi ya kigaidi yanayopata mafunzo nchini humo.

0 comments:

Post a Comment

Translate

facebook

TANGAZA HAPA

KWA HABARI MAKINI

Napokea maoni muhimu kwa pale unapoona apakustahili kuwepo kwenye blogg yetu makini yenye lengo la kukuunganisha pamoja na kuelimishana kwa yale mazuri yote piga simu kwa chochote muhimu namba zipo apo juu

NEWS