Tuesday, 30 September 2014

Hamas yakataa kuzungumza moja kwa moja na Israel
Naibu Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema kuwa, harakati hiyo inasisitiza upinzani wake dhidi ya mazungumzo ya moja kwa moja na utawala wa Kizayuni wa Israel. Mousa Abu Marzouk amesisitiza kwamba, Wapalestina wote wanapinga mazungumzo ya mamlaka ya ndani ya Palestina na utawala haramu wa Israel; kwani wanatambua wazi kuwa, mazungumzo hayo hayawezi kuwa na natija ya maana. Mussa Abu Marzouk ambaye ni kiongozi mwandamizi wa harakati ya Hamas ya Palestina amesema kuwa, makubaliano ya harakati yao ya Fat'h yako wazi na hayana utata. Ameongeza kuwa, jukumu muhimu kabisa la mamlaka ya ndani ya Palestina ni kuitisha uchaguzi na kwamba, Hamas iko tayari kushiriki katika uchaguzi wowote ukiwemo ule wa Bunge. Mwezi Juni mwaka huu serikali ya umoja wa kitaifa iliundwa Palestina kufuatia makubaliano yaliyotiwa saini kati ya Hamas na Fat'h Aprili 23 mwaka huu.

0 comments:

Post a Comment

Translate

facebook

TANGAZA HAPA

KWA HABARI MAKINI

Napokea maoni muhimu kwa pale unapoona apakustahili kuwepo kwenye blogg yetu makini yenye lengo la kukuunganisha pamoja na kuelimishana kwa yale mazuri yote piga simu kwa chochote muhimu namba zipo apo juu

NEWS