Wednesday, 20 January 2016

Umoja wa Mataifa umetaka kutolewa msaada wa zaidi ya dola bilioni moja kwa ajili ya Sudan.
Eugene Owusu, Mratibu wa oparesheni za misaada ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini Jumanne wiki hii amesema kuwa kwa uchache msaada wa fedha wa dola bilioni moja na laki tatu unahitajika kwa ajili ya kuwasaidia raia zaidi ya milioni tano wa Sudan Kusini ambao wanakabiliwa na hali ngumu. Owusu ameongeza kuwa katika kila watu kumi nchini Sudan Kusini, watu wawili walizikimbia nyumba zao miaka miwili iliyopita kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe na mapigano kati ya serikali ya waasi wa nchi hiyo. Mratibu wa oparesheni za misaada ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini amesisitiza kuwa umoja huo unakabiliwa na changamoto kubwa nchini humo.
Watu zaidi ya elfu kumi wameuliwa na wengine zaidi ya milioni mbili na laki tatu wamekuwa wakimbizi tangu kuzuka mapigano huko Sudan Kusini mwezi Disemba mwaka 2013
sos Thran

0 comments:

Post a Comment

Translate

facebook

TANGAZA HAPA

KWA HABARI MAKINI

Napokea maoni muhimu kwa pale unapoona apakustahili kuwepo kwenye blogg yetu makini yenye lengo la kukuunganisha pamoja na kuelimishana kwa yale mazuri yote piga simu kwa chochote muhimu namba zipo apo juu

NEWS