Sunday, 12 April 2015

watu 9 wauliwa katika machafuko ya uchaguzi NigeriaWatu tisa wameuawa kwenye ghasia na maandamano huko kusini mwa Nigeria, wakati nchi hiyo ikiwa imeendesha chaguzi za magavana wa majimbo. Machafuko hayo yaliripotiwa jana, ambapo mengi yalishuhudiwa katika jimbo la Rivers ambalo ni tajiri kwa mafuta. Dakuku Peterside mgombea wa upinzani kutoka chama cha APC amesema kuwa wafuasi wake wanane wameuawa, huku duru za polisi zikisema kuwa afisa mmoja pia amepoteza maisha kwenye ghasia hizo. Ripoti zinasema kuwa, ufyatuaji risasi ulisikika pia katika miji kadhaa katika jimbo la Rivers. Kituo cha kupigia kura na nyumba ya Manuela George-Izunwa, Kamishna wa jimbo la Rivers anayehusika na masuala ya wanawake vimechomwa moto pia. Mawakala wa uchaguzi karibu kumi walitekwa nyara mapema jana huku maelfu ya waandamanaji huko Port Harcourt makao makuu ya jimbo la Rivers, wakiichelewesha kufunguliwa vituo vya kupigia kura.
 
Jiunge nasi pia

www. facebook.com /millanzy.blogspot.com

www.twitter.com / millanzy.blogspot.com








0 comments:

Post a Comment

Translate

facebook

TANGAZA HAPA

KWA HABARI MAKINI

Napokea maoni muhimu kwa pale unapoona apakustahili kuwepo kwenye blogg yetu makini yenye lengo la kukuunganisha pamoja na kuelimishana kwa yale mazuri yote piga simu kwa chochote muhimu namba zipo apo juu

NEWS