Mwanafunzi mmoja wa Mkenya ameaga dunia na wengine zaidi ya 100
kujeruhiwa wakati wakikimbia, baada ya transfoma ya umeme kuripuka
katika bweni moja la wanachuo katika Chuo Kikuu cha Nairobi kabla ya
alfajiri ya leo. Mripuko huo uliibua wasiwasi na wahaka katika mabweni
ya wanachuo wakidhani kuwa wamevamiwa. Katika tuki hilo lililotokea
mapema leo, baadhi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Nairobi waliruka
madirishani ili kujinusuru, ikiwa zimepita siku chache tu baada ya
wanamgambo wa kundi la kigaidi la al Shabab kukishambulia Chuo Kikuu cha
Garissa na kuuwa wanafunzi zaidi ya 100. Peter Mbithi, Makamu Mkuu wa
Chuo Kikuu cha Nairobi amesema kuwa, mwanafunzi aliyefariki dunia
alikuwa kati ya wale walioruka kutoka kwenye bweni lao lililoko katika
ghorofa tano, wakihofia majengo ya chuo hicho yamevamiwa. Walioshuhudia
mripuko huo wa transfoma ya umeme wamesema kuwa iliripuka saa 10.30
alfajiri ya leo kwa saa za Kenya na hivyo kusababisha wanafunzi wa kike
kuanza kupiga kelele na hofu hiyo kuenea pia kwa upande wa wavulana, na
kisha wanafunzi wakaamka na kuanza kujaribu kutoka nje.
Sunday, 12 April 2015
Related Posts:
vita vyaanza upya Sudani Kusini Mapigano makali yameanza tena kati ya majeshi ya serikali ya Sudan Kusini na waasi wa nchi hiyo, ikiwa yamepita chini ya masaa 48 tokea yalipofanyika mazungumzo ya amani kati ya pande hizo mbili.Msemaji wa kundi la… Read More
DOWNLOAD NA SIKILIZA WIMBO MPYA WA DINI KUTOKA KWA MWAMUZIKI Michael Jose KUWA WA KWANZA SASAph Michael Joseph ameleta mapinduzi kwenye tasnia hii ya muziki wa Injili na kujizolea mashabiki kwa muda mfupi sana akiongea kwa mala nyingine kwenye maojiano Prais Pawer Radio alisema najisia faraja sana kuona mashabiki w… Read More
Polisi yachunguza tuhuma za ufisadi dhidi ya Zuma Polisi nchini Afrika Kusini imesema inachunguza tuhuma za ufisadi dhidi ya Rais wa nchi hiyo, Jacob Zuma. Taarifa ya polisi kwa Bunge imekiri kwamba uchunguzi huo umeanzishwa na unajikita zaidi katika madai kwamba, Rais… Read More
UN: Serikali ya Burundi izungumze na wapinzani Umoja wa Mataifa umetaka kutayarishwa anga nzuri ya kufanyika mazungumzo kati ya wanasiasa, vyama vya kisiasa na viongozi wa serikali ya Burundi.Mshauri Maalumu wa Umoja wa Maaifa anayeshughulikia masuala ya kuzuia… Read More
ICC yaitaka Ivory Coast imkabidhi Simone Gbagbo Majaji wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC wameitaka serikali ya Ivory Coast imkabidhi kwenye korti hiyo Simone Gbagbo, mke wa rais wa zamani wa nchi hiyo, ili akashtakiwe kutokana na tuhuma zinazomkabili.… Read More
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment