Chama tawala nchini Nigeria cha PDP kimemkosoa Attahiru Jega
Mkuu wa tume ya uchaguzi ya Nigeria
amesema kuwa hatojiuzulu na amepinga mwito wa baadhi ya wafuasi wa Rais
Goodluck Jonathan wa nchi hiyo waliomtaka ajiuzulu kabla ya uchaguzi
mkuu uliopangwa kufanyika tarehe 28 mwezi huu.
Chama tawala nchini Nigeria cha PDP
kimemkosoa Attahiru Jega kuhusu namna anavyosimamia mchakato wa uchaguzi
huku baadhi wakimtuhumu mkuu huyo wa tume ya uchaguzi ya Nigeria kwa
kumpendelea Muhammad Buhari mtawala wa zamani wa kijeshi wa nchi hiyo
ambaye ni mgombea wa kiti cha urais wa chama cha upinzani cha APC,
tuhuma ambazo amezipinga.
Baadhi ya wafuasi wa Jonathan wametuma
matangazo magazetini wakimtuhumu mkuu wa tume ya uchaguzi ya Nigeria
kuwa anaitumbukiza nchi katika mgogoro kwa kushindwa kutengeneza na
kugawa kwa wakati kadi za kupigia kura.
0 comments:
Post a Comment