Afisa wa ngazi ya juu wa Ujerumani ametaka kuangaliwa upya sera
za Ujerumani za kuiuzia silaha Saudi Arabia akiitaja nchi hiyo ya
kifalme kuwa inaongoza kwa kutuma magaidi katika eneo la Mashariki ya
Kati. Claudia Roth Makamu Mwenyekiti wa bunge la Ujerumani (Bundestag)
amewasilisha ombi hilo wakati alipofanya mahojiano na gazeti la
Ujerumani la Welt am Sonntag. Makamu Mwenyekiti wa bunge la Ujerumani
ameitaja Riyadh kuwa ni mtumaji mkuu wua magaidi Mashariki ya Kati na
kuongeza kuwa, idadi kubwa ya wanamgambo wenye misimamo mikali walioko
Syria, Afghanistan na Iraq wametoka Saudi Arabia. Claudia Roth
mwanasiasa wa chama cha Kijani cha nchini Ujerumani ametaka pia kuachiwa
huru mwanaharakati Msaudia Raif Badawi ambaye amehukumiwa kifungo cha
miaka kumi jela na viboko 1000. Saudi Arabia ni moja ya nchi wanunuzi
wakuu wa silaha za Ujerumani.
Sunday, 8 March 2015
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment