Waziri mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, atalihutubia Bunge la Marekani Jumanne katika hotuba inayosubiriwa kwa hamu kubwa.
Awali, Netanyahu alisema Marekani, na Israel, zinakubaliana kwamba
kuna haja ya kuizuia Iran kuwa na silaha za nyuklia lakini hazikubaliani
namna ya kufikia lengo hilo.
Kauli hiyo ilitolewa siku moja kabla ya waziri mkuu huyo kuhutubia bunge la Marekani.
Mwaliko wa kulihutubiua Bunge umezusha utata Marekani kwa sababu
unafanyika bila ya utamaduni wa kawaida wa kushauriana na White House.
Hatua hiyo imeonyesha mvutano wa uhusiano uliopo baina ya bwana Netanyahu, na rais wa Marekani, Barack Obama.
Bwana Netanyahu anasema kutokukubaliana na Marekani, kunatokana na
mitazamo tofauti kwa sababu Washington, inawasiwasi na usalama wakati
Israel inahofu na uhai.
Katika mahojiano na shirika la habarfi la Reuters, bwana Obama
amesema utawala wake na serikali ya Israel unatofautiana kwa namna ya
kuiwezesha Iran kutokuwa na nguvu za nyuklia.
0 comments:
Post a Comment