Thursday, 16 April 2015

Wagombea 2 wa kiti cha urais kwenye uchaguzi mkuu nchini Sudan wamejiondoa saa chache kabla ya kumalizika uchaguzi huo wakidai kuwa tume ya uchaguzi imekiuka sheria nyingi ili kutoa mwanya kwa Rais Omar al-Bashir kushinda kiti hicho. Ahmed Radi na Omar Awadh Al-Karim wamesema uamuzi wao wa kujiondoa kwenye kinyang’anyiro cha urais unatokana na kuweko ushahidi wa wazi wa ukiukwaji wa sheria za uchaguzi na aina fulani ya udanganyifu kwa upande wa tume ya uchaguzi ya Sudan. Tume hiyo hapo jana ilitangaza kuongeza siku moja ili kutoa fursa ya watu zaidi kupiga kura. Uchaguzi mkuu wa Sudan ulioanza siku ya Jumatatu ulitarajiwa kumalizika hapo jana lakini umeendelea hadi leo baada ya kuongezwa siku moja ya ziada. Huu ni uchaguzi wa kwanza kufanyika tangu kujitenga Sudan Kusini mwaka 2011.
Kiti cha urais kilikuwa kimewavutia wagombea 15 kabla ya Ahmad Radi na Omar Awadh kujiondoa. Hata hivyo Rais al-Bashir anatarajiwa kushinda tena kiti hicho baada ya vyama vikuu vya upinzani kususia zoezi hilo muhimu.

0 comments:

Post a Comment

Translate

facebook

TANGAZA HAPA

KWA HABARI MAKINI

Napokea maoni muhimu kwa pale unapoona apakustahili kuwepo kwenye blogg yetu makini yenye lengo la kukuunganisha pamoja na kuelimishana kwa yale mazuri yote piga simu kwa chochote muhimu namba zipo apo juu

NEWS