Anaitwa Patrick Ole Sosopi. Ni mmasai aliyezaliwa na kukulia mkoa Iringa, jimbo la Ismani. Ana umri wa miaka 28. Ni msomi wa shahada ya kwanza ya Biashara na utawala (rasilimali watu) kutoka chuo kikuu cha Ruaha (RUCO). Kwa sasa kazi zake ni kufuga ng’ombe. Ni Baba wa mke mmoja na mtoto mmoja. Ni mgombea wa nafasi ya umakamu mwenyekiti wa BAVICHA Bara- Taifa. Historia yake ya uongozi na uadilifu wake umekuwa hauna shaka katika vipindi mbalimbali vya maisha yake. Historia yake ya uongozi ilianzia akiwa shule ya msingi, sekondari hadi chuo kikuu cha RUCO ambapo alikuwa waziri wa Fedha kwenye serikali ya wanafunzi 2011/2012. Alijiunga rasmi na CHADEMA mwaka 2009 alipokuwa mwanafunzi wa mwaka wa kwanza akiamini ni chama pekee ambacho kina tija ya kuboresha maisha ya jamii yake ya kimasai na changamoto mbalimbali ambazo zilikuwa zikiwakabili. Ole Sosopi ni mojawapo wa waanzilishi wa CHASO mkoani Iringa, harakati zake katika jimbo la Ismani na mkoa wa Iringa kwa ujumla kila mtu anazijua.

0 comments:
Post a Comment